Mwanzo 17:3-8 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Hapo Abramu akasujudu. Naye Mungu akamwambia,

4. “Ninafanya agano hili nawe: Utakuwa baba wa mataifa mengi.

5. Tangu sasa, hutaitwa tena Abramu, bali utaitwa Abrahamu, maana nimekufanya kuwa baba wa mataifa mengi.

6. Nitakufanya uwe na wazawa wengi sana; kwako nitazusha mataifa mengi na wafalme.

7. Nitalithibitisha agano langu nawe, wazawa wako na vizazi vyao vyote milele; tena nitakuwa Mungu wako na Mungu wa wazawa wako milele.

8. Nitakupa wewe na wazawa wako nchi hii ambamo unaishi kama mgeni; yaani nchi yote ya Kanaani iwe mali yenu milele; nami nitakuwa Mungu wao.”

Mwanzo 17