10. Wafuatao ni wazawa wa Shemu. Miaka miwili baada ya ile gharika, Shemu akiwa na umri wa miaka 100, alimzaa Arfaksadi.
11. Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.
12. Arfaksadi alipokuwa na umri wa miaka 35, alimzaa Shela.
13. Baada ya kumzaa Shela, Arfaksadi aliishi miaka 403 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.
14. Shela alipokuwa na umri wa miaka 30, alimzaa Eberi.
15. Baada ya kumzaa Eberi, Shela aliishi miaka 403 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.
16. Eberi alipokuwa na umri wa miaka 34, alimzaa Pelegi.
17. Baada ya kumzaa Pelegi, Eberi aliishi miaka 430 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.
18. Pelegi alipokuwa na umri wa miaka 30, alimzaa Reu.
19. Baada ya kumzaa Reu, Pelegi aliishi miaka 209 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.
20. Reu alipokuwa na umri wa miaka 32, alimzaa Serugi.
21. Baada ya kumzaa Serugi, Reu aliishi miaka 207 na kupata watoto wengine wa kiume na wa kike.