Mwanzo 10:17-22 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Wahivi, Waarki, Wasini,

18. Waarvadi, Wasemari na Wahamathi. Baadaye watu wa jamii mbalimbali za Kanaani walitawanyika,

19. hata eneo la nchi yao likawa toka Sidoni kuelekea kusini, hadi Gerari mpaka Gaza, na kuelekea mashariki hadi Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu hadi Lasha.

20. Hao ndio wazawa wa Hamu kadiri ya makabila yao, lugha zao, nchi zao na mataifa yao.

21. Shemu, mkubwa wa Yafethi, alikuwa baba yao Waebrania wote.

22. Watoto wa kiume wa Shemu walikuwa Elamu, Ashuru, Arfaksadi, Ludi na Aramu.

Mwanzo 10