Mwanzo 1:3-8 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Mungu akasema, “Mwanga uwe.” Mwanga ukawa.

4. Mungu akauona mwanga kuwa ni mwema. Kisha Mungu akautenganisha mwanga na giza,

5. mwanga akauita “Mchana” na giza akaliita “Usiku.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya kwanza.

6. Mungu akasema, “Anga liwe katikati ya maji, liyatenge maji sehemu mbili.”

7. Mungu akalifanya anga, akayatenga maji yaliyo juu ya anga na yale yaliyo chini ya anga hilo. Ikawa hivyo.

8. Mungu akaliita anga “Mbingu.” Ikawa jioni, ikawa asubuhi; siku ya pili.

Mwanzo 1