Mhubiri 2:5-9 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Nilijifanyia bustani na viunga, nikapanda miti ya matunda ya kila aina.

6. Nilijichimbia mabwawa ya maji ya kumwagilia hiyo miti.

7. Nilinunua watumwa, wanawake kwa wanaume, na wengine wakazaliwa nyumbani mwangu. Nilikuwa na mali nyingi, makundi ya ng'ombe na kondoo wengi kuliko mtu yeyote aliyenitangulia kukaa Yerusalemu.

8. Nilijirundikia fedha na dhahabu kutoka hazina za wafalme na toka mikoani, nami nilipata waimbaji wanaume kwa wanawake, na masuria watamaniwao.

9. Naam, nikawa mkuu, mkuu kuwapita wote waliopata kuwako Yerusalemu kabla yangu; na hekima yangu ikakaa ndani mwangu.

Mhubiri 2