9. Kwa mtu mwelewa kila kitu ni wazi,kwa mwenye maarifa yote ni sawa.
10. Chagua mafundisho yangu badala ya fedha;na maarifa badala ya dhahabu safi.
11. “Mimi Hekima nina thamani kuliko johari;chochote unachotamani hakiwezi kulingana nami.
12. Mimi Hekima ninao ujuzi;ninayo maarifa na busara.
13. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu.Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya;nachukia na lugha mbaya.
14. Nina uwezo wa kushauri na nina hekima.Ninao ujuzi na nina nguvu.
15. Kwa msaada wangu wafalme hutawala,watawala huamua yaliyo ya haki.