Methali 8:9-15 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Kwa mtu mwelewa kila kitu ni wazi,kwa mwenye maarifa yote ni sawa.

10. Chagua mafundisho yangu badala ya fedha;na maarifa badala ya dhahabu safi.

11. “Mimi Hekima nina thamani kuliko johari;chochote unachotamani hakiwezi kulingana nami.

12. Mimi Hekima ninao ujuzi;ninayo maarifa na busara.

13. Kumcha Mwenyezi-Mungu ni kuchukia uovu.Nachukia kiburi, majivuno na maisha mabaya;nachukia na lugha mbaya.

14. Nina uwezo wa kushauri na nina hekima.Ninao ujuzi na nina nguvu.

15. Kwa msaada wangu wafalme hutawala,watawala huamua yaliyo ya haki.

Methali 8