Methali 8:33-36 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Sikilizeni mafunzo mpate hekima,wala msiyakatae.

34. Heri mtu anayenisikiliza,anayekaa kila siku mlangoni pangu,anayekesha karibu na milango yangu.

35. Anayenipata mimi amepata uhai,amepata upendeleo kwa Mwenyezi-Mungu.

36. Asiyenipata anajidhuru mwenyewe;wote wanaonichukia wanapenda kifo.”

Methali 8