1. Sikilizeni! Hekima anaita!Busara anapaza sauti yake!
2. Juu penye mwinuko karibu na njia,katika njia panda ndipo alipojiweka.
3. Karibu na malango ya kuingilia mjini,mahali wanapoingia watu anaita kwa sauti:
4. “Enyi watu wote, nawaita nyinyi!Wito wangu ni kwa ajili ya binadamu.
5. Enyi wajinga, jifunzeni kuwa na akili;sikilizeni kwa makini enyi wapumbavu.
6. Sikilizeni maana nitakachosema ni jambo muhimu;midomoni mwangu mtatoka mambo ya adili.