4. Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.
5. Vitakulinda mbali na mwanamke mbaya,vitakuepusha na maneno matamu ya mwanamke mgeni.
6. Siku moja dirishani mwa nyumba yangu,nilichungulia nje kupitia viunzi vya dirisha,
7. nikawaona vijana wengi wajinga,na mmoja hasa aliyekuwa mpumbavu.