Methali 7:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwanangu, yashike maneno yangu,zihifadhi kwako amri zangu.

2. Zifuate amri zangu nawe utaishi;yalinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.

3. Yafunge vidoleni mwako;yaandike moyoni mwako.

4. Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.

Methali 7