1. Mwanangu, yashike maneno yangu,zihifadhi kwako amri zangu.
2. Zifuate amri zangu nawe utaishi;yalinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
3. Yafunge vidoleni mwako;yaandike moyoni mwako.
4. Iambie Hekima: “Wewe ni dada yangu”,na Busara “Wewe ni rafiki yangu”.