6. Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.
7. Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;
8. lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.
9. Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?Utaamka lini katika usingizi wako?
10. Wasema: “Acha nilale kidogo tu,acha nisinzie kidogo!Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”
11. Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,ufukara utakufuata kama jambazi.