Methali 6:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Ewe mvivu! Hebu ukamchungulie sisimizi,fikiria namna yake ya kuishi ukapate hekima.

7. Sisimizi hana kiongozi, ofisa, wala mtawala;

8. lakini hujiwekea chakula wakati wa kiangazi,hujikusanyia akiba wakati wa mavuno.

9. Ewe mvivu, utalala hapo mpaka lini?Utaamka lini katika usingizi wako?

10. Wasema: “Acha nilale kidogo tu,acha nisinzie kidogo!Niache nikunje mikono nipumzike kidogo!”

11. Wakati huo umaskini utakuvamia kama mnyanganyi,ufukara utakufuata kama jambazi.

Methali 6