26. Mtu hupoteza kipande cha mkate kwa malaya,lakini kwa mke wa mtu mwingine utapoteza uhai wako wote.
27. Je, waweza kuweka moto kifuanina nguo zako zisiungue?
28. Je, waweza kukanyaga makaa ya motona nyayo zako zisiungue?
29. Ndivyo alivyo mwanamume alalaye na mke wa mwenzake;yeyote anayemgusa mwanamke huyo hataacha kuadhibiwa.
30. Watu hawambezi sana mtu akiiba kwa sababu ya njaa;
31. lakini akipatikana lazima alipe mara saba;tena atatoa mali yote aliyo nayo.
32. Mwanamume anayezini na mke wa mtu hana akili kabisa;huyo hujiangamiza yeye mwenyewe.