Methali 5:6-17 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Yeye haijali njia ya uhai,njia zake ni za kutangatanga, wala hajui.

7. Sasa enyi wanangu, nisikilizeni,wala msisahau maneno ya kinywa changu.

8. Iepushe njia yako mbali naye,wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.

9. Usije ukawapa wengine heshima yako,na wakatili miaka yako;

10. wageni wasije wakajishibisha kwa mali yako,na jasho lako likaishia nyumbani kwa mgeni.

11. Mwishoni mwa maisha yako utaombolezawakati mwili wako utakapoangamizwa.

12. Hapo utasema, “Jinsi gani nilivyochukia nidhamu,na kudharau maonyo moyoni mwangu!

13. Sikuisikiliza sauti ya waalimu wangu,wala kuwategea sikio wakufunzi wangu.

14. Sasa niko karibu kuangamia kabisambali na jumuiya ya watu.”

15. Mkeo ni kama kisima cha maji safi:Kunywa maji ya kisima chako mwenyewe.

16. Ya nini chemchemi zako zitawanywe mbali,na vijito vya maji barabarani?

17. Hiyo ni yako wewe mwenyewe,wala usiwashirikishe watu wengine.

Methali 5