2. Maana ninawapa maagizo mema,msiyakatae mafundisho yangu.
3. Mimi pia nilikuwa mtoto mwenye baba,nilikuwa mpole, kipenzi cha mama yangu.
4. Baba yangu alinifundisha hiki:“Zingatia kwa moyo maneno yangu,shika amri zangu nawe utaishi.
5. Jipatie hekima, jipatie ufahamu;usisahau wala kupuuza maneno yangu.
6. Usimwache Hekima, naye atakutunza;umpende, naye atakulinda.
7. Jambo la msingi ni kujipatia hekima;toa vyote ulivyonavyo ujipatie akili.
8. Mthamini sana Hekima, naye atakutukuza;ukimshikilia atakupa heshima.
9. Atakuvika kilemba kizuri kichwani pako,atakupa taji maridadi.”
10. Mwanangu, sikia na kuyapokea maneno yangu,ili upate kuwa na miaka mingi ya kuishi.