12. Kamwe hamtendei mumewe mabaya,bali humtendea mema maisha yake yote.
13. Hutafuta sufu na kitani,na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.
14. Yeye ni kama meli za biashara:Huleta chakula chake kutoka mbali.
15. Huamka kabla ya mapambazuko,akaitayarishia jamaa yake chakula,na kuwagawia kazi watumishi wake.
16. Hufikiria kununua shamba, kisha hulinunua,na kulima zabibu kwa faida ya jasho lake.