11. Mumewe humwamini kwa moyo,kwake atapata faida daima.
12. Kamwe hamtendei mumewe mabaya,bali humtendea mema maisha yake yote.
13. Hutafuta sufu na kitani,na kufanya kazi kwa mikono yake kwa bidii.
14. Yeye ni kama meli za biashara:Huleta chakula chake kutoka mbali.
15. Huamka kabla ya mapambazuko,akaitayarishia jamaa yake chakula,na kuwagawia kazi watumishi wake.