Methali 30:26-33 Biblia Habari Njema (BHN)

26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;

27. nzige: Hawana mfalme,lakini wote huenda pamoja kwa vikosi;

28. mjusi: Waweza kumshika mkononi,lakini huingia katika ikulu.

29. Kuna viumbe vitatu vyenye mwendo wa kupendeza,naam, kuna viumbe vinne vyenye mwendo mzuri;

30. simba: Mnyama mwenye nguvu kuliko wote,wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;

31. jogoo aendaye kwa maringo;tena beberu;na mfalme mbele ya watu wake.

32. Kama umekuwa mpumbavu hata ukajisifu,au kama umekuwa unapanga maovu,chunga mdomo wako.

33. Maana ukisukasuka maziwa utapata siagi,ukimpiga mtu pua atatoka damu;kadhalika kuchochea hasira huleta ugomvi.

Methali 30