Methali 30:18-30 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,naam, mambo manne nisiyoyaelewa:

19. Njia ya tai angani,njia ya nyoka mwambani,njia ya meli baharini,na kinachomvuta mwanamume kwa mwanamke.

20. Mwenendo wa mwanamke mwasherati ni hivi:Yeye hula, akajipangusa mdomo,na kusema, “Sijafanya kosa lolote!”

21. Kuna mambo matatu ambayo huitetemesha dunia,naam, mambo manne ambayo haiwezi kuyastahimili:

22. Mtumwa anayekuwa mfalme;mpumbavu anayeshiba chakula;

23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.

24. Kuna viumbe vinne vidogo sana duniani,lakini vina akili sana:

25. Sisimizi: Wadudu wasio na nguvu,lakini hujihifadhia chakula wakati wa kiangazi;

26. pelele: Wanyama wasio na uwezo,lakini hujitengenezea makao miambani;

27. nzige: Hawana mfalme,lakini wote huenda pamoja kwa vikosi;

28. mjusi: Waweza kumshika mkononi,lakini huingia katika ikulu.

29. Kuna viumbe vitatu vyenye mwendo wa kupendeza,naam, kuna viumbe vinne vyenye mwendo mzuri;

30. simba: Mnyama mwenye nguvu kuliko wote,wala hamwogopi mnyama mwingine yeyote;

Methali 30