16. Kuzimu,tumbo la mwanamke lisilozaa,ardhi isiyoshiba maji,na moto usiosema, “Imetosha!”
17. Kama mtu akimdhihaki baba yake,na kudharau utii kwa mama yake,kunguru wa bondeni watamdonoa macho,na kuliwa na tai.
18. Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu,naam, mambo manne nisiyoyaelewa:
19. Njia ya tai angani,njia ya nyoka mwambani,njia ya meli baharini,na kinachomvuta mwanamume kwa mwanamke.
20. Mwenendo wa mwanamke mwasherati ni hivi:Yeye hula, akajipangusa mdomo,na kusema, “Sijafanya kosa lolote!”
21. Kuna mambo matatu ambayo huitetemesha dunia,naam, mambo manne ambayo haiwezi kuyastahimili:
22. Mtumwa anayekuwa mfalme;mpumbavu anayeshiba chakula;
23. mwanamke asiyependwa anayeolewa;na mjakazi achukuapo nafasi ya bibi yake.