25. Usiogope juu ya tishio la ghafla,wala shambulio kutoka kwa waovu,
26. Maana Mwenyezi-Mungu ndiye atakayekutegemeza;atakuepusha usije ukanaswa mtegoni.
27. Usimnyime mtu anayehitaji msaada,ikiwa unao uwezo wa kufanya hivyo.
28. Usimwambie jirani yako aende zake hadi kesho,hali wewe waweza kumpa anachohitaji leo.