Methali 3:25-28 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Usiogope juu ya tishio la ghafla,wala shambulio kutoka kwa waovu,

26. Maana Mwenyezi-Mungu ndiye atakayekutegemeza;atakuepusha usije ukanaswa mtegoni.

27. Usimnyime mtu anayehitaji msaada,ikiwa unao uwezo wa kufanya hivyo.

28. Usimwambie jirani yako aende zake hadi kesho,hali wewe waweza kumpa anachohitaji leo.

Methali 3