9. Mwenye hekima akibishana na mpumbavu,mpumbavu huwaka hasira na kucheka bila kutulia.
10. Wapendao kumwaga damu humchukia mtu asiye na hatia,lakini watu wema huyalinda maisha yake.
11. Mpumbavu huonesha hasira yake wazi,lakini mwenye hekima huizuia na kuituliza.
12. Mtawala akisikiliza mambo ya uongo,maofisa wake wote watakuwa waovu.