Methali 29:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Mfalme akitumia haki huipatia nchi uthabiti,lakini akipenda hongo taifa huangamia.

5. Mwenye kumbembeleza jirani yake,anatega mtego wa kujinasa mwenyewe.

6. Mtu mbaya hunaswa kwa kosa lake,lakini mtu mwadilifu huimba na kufurahi.

7. Mwadilifu anajua haki za maskini,lakini mtu mwovu hajui mambo hayo.

8. Wenye dharau huutia vurugu mji mzima,lakini wenye hekima hutuliza ghadhabu.

Methali 29