Methali 29:23-27 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe,lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.

24. Anayeshirikiana na mwizi anajidhuru mwenyewe;husikia laana ya aliyeonewa bila kusema neno.

25. Kuwaogopa watu ni kujitega mwenyewe,lakini anayemtumaini Mwenyezi-Mungu yu salama.

26. Wengi hupenda kujipendekeza kwa mtawala,hali mtu hupata haki yake kwa Mwenyezi-Mungu.

27. Mdhalimu ni chukizo kwa mnyofu,naye mnyofu ni chukizo kwa mwovu.

Methali 29