22. Mwenye ghadhabu huchochea ugomvi,mtu wa hasira husababisha makosa mengi.
23. Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe,lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.
24. Anayeshirikiana na mwizi anajidhuru mwenyewe;husikia laana ya aliyeonewa bila kusema neno.
25. Kuwaogopa watu ni kujitega mwenyewe,lakini anayemtumaini Mwenyezi-Mungu yu salama.
26. Wengi hupenda kujipendekeza kwa mtawala,hali mtu hupata haki yake kwa Mwenyezi-Mungu.
27. Mdhalimu ni chukizo kwa mnyofu,naye mnyofu ni chukizo kwa mwovu.