Methali 29:15-24 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Adhabu na maonyo huleta hekima,lakini mtoto aliyeachwa afanye apendavyo humwaibisha mama yake.

16. Waovu wakitawala maovu huongezeka,lakini waadilifu watashuhudia kuanguka kwao.

17. Mpe nidhamu mwanao naye hatakupa wasiwasi;yeye ataufurahisha moyo wako.

18. Pasipo maono ya kinabii watu hukosa nidhamu;heri mtu yule anayeshika sheria.

19. Mtumwa haonyeki kwa maneno matupu,maana ingawa anayaelewa yeye hatayatii.

20. Wamwona mtu apayukaye bila kufikiri?Mtu mpumbavu ni afadhali kuliko yeye.

21. Ambembelezaye mtumwa wake tangu utoto,mwishowe mtumwa huyo atamrithi.

22. Mwenye ghadhabu huchochea ugomvi,mtu wa hasira husababisha makosa mengi.

23. Kiburi cha mtu humporomosha mwenyewe,lakini mnyenyekevu wa roho atapata heshima.

24. Anayeshirikiana na mwizi anajidhuru mwenyewe;husikia laana ya aliyeonewa bila kusema neno.

Methali 29