Methali 29:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Anayeonywa mara nyingi akawa mkaidi,ataangamia ghafla asipone tena.

2. Waadilifu wakitawala watu hufurahi,lakini waovu wakitawala watu hulalamika.

3. Apendaye hekima humfurahisha baba yake;lakini aandamanaye na malaya hufuja mali yake.

Methali 29