Methali 28:25-28 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Mchoyo huchochea ugomvi,lakini anayemtegemea Mwenyezi-Mungu atafanikiwa.

26. Anayetegemea akili yake mwenyewe ni mpumbavu;lakini anayeishi kwa hekima atakuwa salama.

27. Aliye mkarimu kwa maskini hatatindikiwa kitu,lakini anayekataa kuwaangalia atalaaniwa kwa wingi.

28. Waovu wakitawala watu hujificha,lakini wakiangamia, waadilifu huongezeka.

Methali 28