Methali 28:12-19 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Watu wema wakipata madaraka maisha hufana,lakini waovu wakitawala watu hujificha.

13. Afichaye makosa yake hatafanikiwa;lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema.

14. Heri mtu amchaye Mwenyezi-Mungu daima;lakini mkaidi wa moyo ataangukia maafa.

15. Mtawala mwovu anayewatawala maskini,ni kama simba angurumaye au dubu anayeshambulia.

16. Mtawala asiye na akili ni mdhalimu mkatili;lakini achukiaye mali ya udanganyifu atatawala muda mrefu.

17. Mtu anayelemewa na hatia ya kuua mtu,atakuwa mkimbizi mpaka kaburini;mtu yeyote na asijaribu kumzuia.

18. Aishiye kwa unyofu atasalimishwa,lakini mdanganyifu ataanguka kabisa.

19. Anayelima shamba lake atapata chakula kingi,bali anayefuata yasiyofaa atapata umaskini tele.

Methali 28