13. Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni, chukua nguo yake;mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.
14. Amwamkiaye jirani kwa kelele alfajiri,itaeleweka kwamba amemtakia laana.
15. Mke mgomvi daima,ni sawa na tonatona ya maji siku ya mvua.
16. Kumzuia ni sawa na kuzuia upepo,au kukamata mafuta kwa mkono.
17. Chuma hunoa chuma,kadhalika mtu hufundishwa na wenzake.
18. Anayeutunza mtini hula tini,anayemhudumia bwana wake ataheshimiwa.
19. Kama uso ujionavyo wenyewe majini,ndivyo ujijuavyo mwenyewe moyoni.
20. Kuzimu na Uharibifu kamwe havishibi,kadhalika na macho ya watu hayashibi.
21. Ubora wa fedha au dhahabu hupimwa kwa moto,na mtu hupimwa kutokana na sifa zake.
22. Mtwange mpumbavu katika kinu pamoja na nafaka,lakini hutafaulu kumtenganisha na upumbavu wake.
23. Angalia vizuri hali ya mifugo yako;tunza vizuri wanyama wako.
24. Maana utajiri haudumu milele,wala taji haidumu vizazi vyote.