12. Mwenye busara huona hatari akajificha,lakini mjinga hujitokeza mbele akaumia.
13. Mtu akiahidi mbele yako kumdhamini mgeni, chukua nguo yake;mfanye awajibike kwa kuwadhamini wageni.
14. Amwamkiaye jirani kwa kelele alfajiri,itaeleweka kwamba amemtakia laana.
15. Mke mgomvi daima,ni sawa na tonatona ya maji siku ya mvua.