Methali 26:24-28 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Mwenye chuki huficha chuki yake kwa maneno mazuri,lakini huwa ana hila moyoni mwake.

25. Akiongea vizuri usimwamini,moyoni mwake mna chuki chungu nzima.

26. Huenda akaficha chuki yake,lakini nia zake mbaya zitajulikana kwa wote.

27. Amchimbiaye mwenzake shimo, hutumbukia mwenyewe;abingirishaye jiwe litamrudia mwenyewe.

28. Asemaye uongo huwachukia hao anaowaumiza,naye abembelezaye huleta maangamizi.

Methali 26