1. Heshima apewayo mpumbavu haimfai;ni kama theluji ya kiangazi,au mvua ya wakati wa mavuno.
2. Kama shomoro au mbayuwayu wasiotua,kadhalika laana asiyostahili mtu haimtui.
3. Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda,na fimbo kwa mgongo wa mpumbavu.
4. Usimjibu mpumbavu kipumbavu,usije ukafanana naye.
5. Mjibu mpumbavu kama ustahilivyo upumbavu wake,asije akajiona kuwa mwenye hekima zaidi.
6. Kumtuma mpumbavu ujumbe,ni kama kujikata miguu au kujitafutia shida.