Methali 23:5-10 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,huwa kama umepata mabawa ghafla,ukaruka na kutowekea angani kama tai.

6. Usile chakula cha mtu bahili,wala usitamani mapochopocho yake,

7. maana moyoni mwake anahesabu unachokula.Atakuambia, “Kula, kunywa!”Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.

8. Utatapika vipande ulivyokula;shukrani zako zote zitakuwa za bure.

9. Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,maana atapuuza hekima ya maneno yako.

10. Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,wala usiingilie mashamba ya yatima,

Methali 23