4. Ikiwa unayo hekima ya kutosha,usijitaabishe kutafuta utajiri.
5. Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,huwa kama umepata mabawa ghafla,ukaruka na kutowekea angani kama tai.
6. Usile chakula cha mtu bahili,wala usitamani mapochopocho yake,
7. maana moyoni mwake anahesabu unachokula.Atakuambia, “Kula, kunywa!”Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.
8. Utatapika vipande ulivyokula;shukrani zako zote zitakuwa za bure.
9. Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,maana atapuuza hekima ya maneno yako.
10. Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,wala usiingilie mashamba ya yatima,
11. maana Mungu, Mkombozi, ni mwenye nguvu,naye ataitetea haki yao dhidi yako.
12. Tumia akili zako kufuata mafundisho;tumia masikio yako kusikiliza maarifa.
13. Usiache kumrudi mtoto;ukimchapa kiboko hatakufa.
14. Ukimtandika kiboko,utayaokoa maisha yake na kuzimu.
15. Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.
16. Moyo wangu utashangilia,mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.
17. Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.
18. Hakika kuna kesho ya milele,na tumaini lako halitakuwa bure.
19. Sikia mwanangu, uwe na hekima;fikiria sana jinsi unavyoishi.
20. Usiwe mmoja wa walevi wa divai,wala walafi wenye kupenda nyama,
21. maana walevi na walafi wataishia kuwa maskini,anayetumia siku yake kusinzia atavaa matambara.
22. Msikilize baba yako aliyekuzaa,wala usimdharau mama yako akizeeka.
23. Nunua ukweli, wala usiuuze;nunua hekima, mafunzo na busara.