30. Ni wale ambao hawabanduki penye divai,wale wakaao chonjo kuonja divai iliyokolezwa.
31. Usiitamani divai hata kwa wekundu wake,hata kama inametameta katika bilauri,na kushuka taratibu unapoinywa.
32. Mwishowe huuma kama nyoka;huchoma kama nyoka mwenye sumu.
33. Macho yako yataona mauzauza,moyo wako utatoa mambo yaliyopotoka.
34. Utakuwa kama mtu alalaye katikati ya bahari,kama mtu alalaye juu ya mlingoti wa meli.