1. Ukiketi kula pamoja na mtawala,usisahau hata kidogo uko pamoja na nani.
2. Zuia sana hamu yako,ikiwa wewe wapenda sana kula.
3. Usitamani vyakula vyake vizuri,maana vyaweza kukudanganya.
4. Ikiwa unayo hekima ya kutosha,usijitaabishe kutafuta utajiri.
5. Kufumba na kufumbua utajiri hutoweka,huwa kama umepata mabawa ghafla,ukaruka na kutowekea angani kama tai.
6. Usile chakula cha mtu bahili,wala usitamani mapochopocho yake,
7. maana moyoni mwake anahesabu unachokula.Atakuambia, “Kula, kunywa!”Lakini moyoni mwake hayuko pamoja nawe.
8. Utatapika vipande ulivyokula;shukrani zako zote zitakuwa za bure.
9. Usiseme maneno yako mbele ya mpumbavu,maana atapuuza hekima ya maneno yako.
10. Usiondoe alama ya mpaka wa zamani,wala usiingilie mashamba ya yatima,
11. maana Mungu, Mkombozi, ni mwenye nguvu,naye ataitetea haki yao dhidi yako.
12. Tumia akili zako kufuata mafundisho;tumia masikio yako kusikiliza maarifa.
13. Usiache kumrudi mtoto;ukimchapa kiboko hatakufa.
14. Ukimtandika kiboko,utayaokoa maisha yake na kuzimu.
15. Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara,moyo wangu pia utakuwa wenye furaha.
16. Moyo wangu utashangilia,mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.
17. Moyo wako usiwaonee wivu wenye dhambi,ila endelea kumcha Mwenyezi-Mungu siku zote.