Methali 22:5-11 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Njia ya waovu imejaa miiba na mitego;anayetaka kuhifadhi maisha yake ataiepa.

6. Mfunze mtoto namna ya kuishi vizuri,naye hatasahau njia hiyo hata uzeeni.

7. Tajiri humtawala maskini;mkopaji ni mtumwa wa mkopeshaji.

8. Apandaye dhuluma atavuna janga;uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.

9. Mtu mkarimu atabarikiwa,maana chakula chake humgawia maskini.

10. Mfukuze mwenye dharau na fujo itatoweka,ugomvi na matusi vitakoma.

11. Mwenye nia safi na maneno mazuri,atakuwa rafiki wa mfalme.

Methali 22