Methali 22:11-16 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mwenye nia safi na maneno mazuri,atakuwa rafiki wa mfalme.

12. Mwenyezi-Mungu hulinda elimu ya kweli,lakini huyavuruga maneno ya waovu.

13. Mvivu husema, “Siwezi kutoka nje;kuna simba huko, ataniua!”

14. Kinywa cha mwasherati ni shimo refu;anayechukiwa na Mwenyezi-Mungu atatumbukia humo.

15. Mtoto hupenda mambo ya kijinga moyoni,lakini fimbo ya nidhamu humwondolea hayo.

16. Anayemdhulumu maskini atamfanya afaidike mwishowe,anayewapa matajiri zawadi ataishia kuwa maskini.

Methali 22