Methali 21:5-12 Biblia Habari Njema (BHN)

5. Mipango ya mtu wa bidii huleta mali kwa wingi,lakini kila aliye na pupa huishia patupu.

6. Mali ipatikanayo kwa udanganyifu,ni mvuke upitao na mtego wa kifo.

7. Ukatili wa wakatili utawafutilia mbali,maana wanakataa kutenda yaliyo ya haki.

8. Njia ya mtu mwenye hatia imepotoka,lakini mwenendo wa mnyofu umenyooka.

9. Afadhali kuishi pembeni juu ya paa,kuliko kuishi nyumbani na mwanamke mgomvi.

10. Anachopania kutenda mtu mbaya ni uovu;hata kwa jirani yake hana huruma.

11. Ukimwadhibu mwenye dhihaka, mjinga hupata hekima;ukimfundisha mwenye hekima, unampatia maarifa.

12. Mungu Mwadilifu anajua wanayotenda waovu nyumbani kwao;naye atawaangusha na kuwaangamiza.

Methali 21