1. Moyo wa mfalme ni kama maji yanayotiririka;Mwenyezi-Mungu, huuongoza popote apendapo.
2. Matendo yote ya mtu ni sawa machoni pake,lakini Mwenyezi-Mungu hupima mioyo.
3. Kutenda mambo mema na ya haki,humpendeza Mwenyezi-Mungu kuliko tambiko.
4. Macho ya kiburi na moyo wa majivunohuonesha wazi dhambi ya waovu.
5. Mipango ya mtu wa bidii huleta mali kwa wingi,lakini kila aliye na pupa huishia patupu.