1. Moyo wa mfalme ni kama maji yanayotiririka;Mwenyezi-Mungu, huuongoza popote apendapo.
2. Matendo yote ya mtu ni sawa machoni pake,lakini Mwenyezi-Mungu hupima mioyo.
3. Kutenda mambo mema na ya haki,humpendeza Mwenyezi-Mungu kuliko tambiko.
4. Macho ya kiburi na moyo wa majivunohuonesha wazi dhambi ya waovu.