Methali 20:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.

2. Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.

3. Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;wapumbavu ndio wanaogombana.

4. Mvivu halimi wakati wa kulima;wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.

Methali 20