1. Divai huleta dhihaka na kileo huleta ugomvi;yeyote anayevutiwa navyo hana hekima.
2. Ghadhabu kali ya mfalme ni kama simba angurumaye;anayemkasirisha anayahatarisha maisha yake.
3. Ni jambo la heshima kuepa ugomvi;wapumbavu ndio wanaogombana.
4. Mvivu halimi wakati wa kulima;wakati wa mavuno atatafuta asipate chochote.