Methali 2:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwanangu, ukiyakubali maneno yangu,na kuyathamini maagizo yangu;

2. ukitega sikio lako kusikiliza hekima,na kuuelekeza moyo wako upate ufahamu;

3. naam, ukiomba upewe busara,ukisihi upewe ufahamu;

4. ukiitafuta hekima kama fedha,na kuitaka kama hazina iliyofichika;

5. hapo utaelewa ni nini kumcha Mwenyezi-Mungu,utafahamu maana ya kumjua Mungu.

6. Maana Mwenyezi-Mungu huwapa watu hekima;kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu.

7. Huwawekea wanyofu akiba ya hekima safi,yeye ni ngao kwa watu waishio kwa uaminifu.

Methali 2