3. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
4. Mali huvuta marafiki wengi wapya,lakini maskini huachwa bila rafiki.
5. Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;asemaye uongo hataepa adhabu.
6. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.
7. Maskini huchukiwa na ndugu zake;marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!Hata awabembeleze namna gani hatawapata.