Methali 19:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

2. Haifai mtu kuwa bila akili;mwenda harakaharaka hujikwaa.

3. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

4. Mali huvuta marafiki wengi wapya,lakini maskini huachwa bila rafiki.

Methali 19