1. Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.
2. Haifai mtu kuwa bila akili;mwenda harakaharaka hujikwaa.
3. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
4. Mali huvuta marafiki wengi wapya,lakini maskini huachwa bila rafiki.