Methali 19:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Afadhali maskini aishiye kwa unyofu,kuliko mtu mpotovu wa maneno na mpumbavu.

2. Haifai mtu kuwa bila akili;mwenda harakaharaka hujikwaa.

3. Mtu akijiangamiza kwa upumbavu wake,huielekeza hasira yake dhidi ya Mwenyezi-Mungu.

4. Mali huvuta marafiki wengi wapya,lakini maskini huachwa bila rafiki.

5. Shahidi mwongo hataacha kuadhibiwa;asemaye uongo hataepa adhabu.

6. Watu wengi hujipendekeza kwa wakuu;kila mtu hutaka kuwa rafiki ya mtu mkarimu.

7. Maskini huchukiwa na ndugu zake;marafiki zake ndio zaidi: Humkimbia!Hata awabembeleze namna gani hatawapata.

8. Ajipatiaye hekima anaipenda nafsi yake;anayezingatia busara atastawi.

9. Shahidi mwongo hatakosa kuadhibiwa;asemaye uongo ataangamia.

10. Haifai kwa mpumbavu kuishi kwa anasa,tena ni vibaya zaidi mtumwa kuwatawala wakuu.

Methali 19