1. Anayetafuta yake tu hujitenga na wenzake;hukasirika akipewa shauri lolote jema.
2. Mpumbavu hapendezwi na busara;kwake cha maana ni maoni yake tu.
3. Ajapo mwovu huja pia dharau;pamoja na aibu huja fedheha.
4. Maneno yaweza kuwa chemchemi ya hekima;yenye kilindi kama bahari, kama kijito kinachobubujika.
5. Si vizuri kumpendelea mtu mwovu,na kumnyima haki mtu mwadilifu.
6. Maneno ya mpumbavu huleta ugomvi;kila anachosema husababisha adhabu.
7. Kinywa cha mpumbavu humwangamiza mwenyewe;mdomo wake ni mtego wa kumnasa yeye mwenyewe.