9. Mtu aweza kufanya mipango yake,lakini Mwenyezi-Mungu huongoza hatua zake.
10. Mfalme huamua kwa maongozi ya Mungu;anapotoa hukumu hakosei.
11. Mwenyezi-Mungu hutaka kipimo na mizani halali;mawe yote mfukoni ya kupimia ni kazi yake.
12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.
13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.
14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.
15. Uso wa mfalme ukingaa kuna uhai;wema wake ni kama wingu la masika.
16. Kupata hekima ni bora kuliko dhahabu;kupata akili ni chaguo bora kuliko fedha.