8. Afadhali mali kidogo kwa uadilifu,kuliko mapato mengi kwa udhalimu.
9. Mtu aweza kufanya mipango yake,lakini Mwenyezi-Mungu huongoza hatua zake.
10. Mfalme huamua kwa maongozi ya Mungu;anapotoa hukumu hakosei.
11. Mwenyezi-Mungu hutaka kipimo na mizani halali;mawe yote mfukoni ya kupimia ni kazi yake.
12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.