Methali 16:8-12 Biblia Habari Njema (BHN)

8. Afadhali mali kidogo kwa uadilifu,kuliko mapato mengi kwa udhalimu.

9. Mtu aweza kufanya mipango yake,lakini Mwenyezi-Mungu huongoza hatua zake.

10. Mfalme huamua kwa maongozi ya Mungu;anapotoa hukumu hakosei.

11. Mwenyezi-Mungu hutaka kipimo na mizani halali;mawe yote mfukoni ya kupimia ni kazi yake.

12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.

Methali 16