Methali 16:3-14 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Mwekee Mwenyezi-Mungu kazi yako,nayo mipango yako itafanikiwa.

4. Mwenyezi-Mungu ameumba kila kitu kwa kusudi lake;hata waovu kwa ajili ya siku ya maangamizi.

5. Kila mwenye kiburi ni chukizo kwa Mwenyezi-Mungu;hakika mtu wa namna hiyo hataacha kuadhibiwa.

6. Kwa utii na uaminifu mtu huondolewa dhambi,kwa kumcha Mwenyezi-Mungu huepuka uovu.

7. Mwenyezi-Mungu akipendezwa na mwenendo wa mtu,huwageuza hata adui zake kuwa marafiki.

8. Afadhali mali kidogo kwa uadilifu,kuliko mapato mengi kwa udhalimu.

9. Mtu aweza kufanya mipango yake,lakini Mwenyezi-Mungu huongoza hatua zake.

10. Mfalme huamua kwa maongozi ya Mungu;anapotoa hukumu hakosei.

11. Mwenyezi-Mungu hutaka kipimo na mizani halali;mawe yote mfukoni ya kupimia ni kazi yake.

12. Ni chukizo kubwa wafalme kutenda uovu,maana msingi wa mamlaka yao ni haki.

13. Mfalme hupendelea mtu asemaye kwa unyofu;humpenda mtu asemaye ukweli.

14. Hasira ya mfalme ni kama mjumbe wa kifo;mtu mwenye busara ataituliza.

Methali 16